Tarehe 22 Mei, 2026 ilifanyika "Wine Tasting Festival" Eden Garden Resort mjini Bujumbura iliyoandaliwa na Ubalozi. Lengo la hafla hiyo lilikuwa ni kuutangaza mvinyo wa Tanzania katika soko la Burundi.
Hafla hiyo iliwakutanisha watengenezaji na wauzaji wa mvinyo kutoka Tanzania, wasambazaji na wauzaji wa mvinyo wa Burundi pamoja na Wanadiplomasia wanaowakilisha nchi na mashirika mbalimbali nchini Burundi.