Maonesho ya Biashara ya Pamoja (Joint Expo) kati ya Tanzania na Burundi yalifanyika kuanzia tarehe 20 hadi 24 Mei, 2026 kwenye Viwanja vya Intwari Bujumbura, Burundi.  Maonesho hayo yalijumuisha wajasiriamali themanini (80) kutoka Mikoa ya  Dodoma, Kigoma, Kigoma, Geita , Mwanza Shinyanga na Tabora   kwa upande wa Tanzania. Mgeni rasmi  alikuwa Mhe. Balozi Simon Sirro, Mkuu wa mkoa wa Kigoma kwa upande wa Tanzania na Upande wa Burundi alikuwa Nigibira Christine, Katibu Mkuu Wizara ya Biashara ambaye alimwakilisha Waziri wa Biashara Mhe. Dkt, Hassan Kibeya. Maonesho hayo yaliandaliwa kwa pamoja kwa kushirikiana na Serikali ya Burundi. Aidha, Maonesho hayo yalihusisha wazalishaji na wasambazaji wakubwa na wadogo wa mvinyo wetu kutoka Dodoma ili kutambulisha mvinyo wa Tanzania katika soko la Burundi ambako haufahamiki vizuri. Wakati wa ufunguzi wa Maonesho hayo yalipambwa na Ngoma ya Asili ya Kirungi Ingoma (drummers) ambayo ni alama, kielelezo na ishara ya uenzi utamaduni wa Kirundi na hutumbuizwa wakati wa ufunguzi wa matukio  makubwa ya kitaifa hususan wanapokuwepo Viongozi wa Serikali.  Aidha, Maadhimisho hayo yalipambwa na Mabanda ya Maonesho  ya Wajasiriamli wa Tanzania na Burundi yaiyokuwa yamesheheni bidhaa mbalimbali kama vile mvinyo, mchele, dawa za asili, batikiv vitenge, asali, bidhaa za usindikaji, samaki wa Tilapia kutoka Mwanza , na bidhaa nyinginezo.

  • Mhe. Gelasius G. Byakanwa, Balozi wa Tanzania nchini Burundi akiwa kwenye picha ya pamoja na mgeni rasmi kwa upande wa Tanzania, Mhe. Balozi Simon Sirro, Mkuu wa Mkoa wa Kigoma na kwa upande wa Burundi, alikuwa ni Katibu Mkuu Wizara ya Biashara Burundi, Nigibira Christine ambaye amemwakilisha Waziri wa Biashara wa Burundi Dkt. Hassan Kibeya, pamoja na viongozi wengine walioshiriki kwenye maonesho hayo.
  • Mhe. Gelasius G. Byakanwa, Balozi wa Tanzania nchini, Balozi wa Tanzania nchini Burundi akipiga ngoma yaAsili ya Kirundi Ingoma (drummers) ambayo ni alama, kielelezo na ishara ya kuenzi utamaduni wa asili wa kirundi i ambayo ilikuwa ikiburudisha wakati wa ufunguzi wa Maonesho. Ngoma hiyo hutumbuizwa wakati wa ufunguzi wa matukio makubwa ya kitaifa hususan wanapokuwepo Viongozi wa Serikali.
  • Muonekano wa mabanda ya Wajasiriamali na watu mbalimbali waliotembelea mabanda hayo na kununua bidhaa mbalimbali za kitanzania.